Monday, November 5, 2012

''KAMPENI CHAFU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI''



Yakiwa yamebaki masaa machache wananchi wa Marekani waanze kupiga kura kumchagua rais wa nchi hiyo kwa awamu nyingine, visa na mikasa ama vituko vimezidi kutawala katika kampeni za uchaguzi huo labda ni mzuka wa kuonesha hisia za watu tofauti tofauti kwa yule wanaemsapoti na kumponda wasiyemsapoti.

Hivi karibuni watu wanaosadikika kuwa ni wapinzani wa rais Obama wametoa toilet paper zenye sura yake na T.P hizo zikasambaa maeneo ya firestation huko Florida.

Ripoti zinasema toilet paper hizo zimetolewa kujibu mashambulizi baada ya mfanyakazi mmoja wa kituo hicho cha zimamoto aliziondoa sticker zote zinazompinga Obama ambazo zilikuwa zimewekwa kwenye maeneo ya umma na sio maeneo ya watu binafsi ama mali binafsi.

Hata hivyo toilet paper hizo nazo zimeondelewa maeneo hayo na kupigwa marufuku maeneo hayo ya Florida firestation kwa sababu ni maeneo ya umma (public place) na sio maeneo binafsi.

No comments:

Post a Comment